Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)

Tanoil Investments Limited

Washirika & Wateja Wetu

Mtendaji Mkuu
Ndugu James Shangari Sanawa

Mtendaji Mkuu

Ujumbe Wa Ukaribisho

Wateja na wadau wetu wa thamani! Tumejipanga kuendesha maendeleo na kuchochea ukuaji wa uchumi nchini Tanzania na katika ukanda wetu. Kama kampuni tanzu inayomilikiwa kwa asilimia 100 na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), jukumu letu ni kushiriki katika mnyororo wa thamani wa biashara ya mafuta katika mkondo wa kati na mkondo wa chini. Tangu kuanzishwa kwetu mwaka 1999 na kufanyiwa maboresho makubwa mwaka 2017, tumekua na kubadilika kuwa kampuni ya nishati inayozingatia misingi ya kibiashara, ikiwa na msingi imara wa ubunifu, uendelevu na utoaji wa huduma bora. Tukiendeshwa na dira yetu isemayo “Kuwa kampuni kinara ya uuzaji wa nishati inayopendelewa, inayofanya kazi ndani na nje ya nchi kwa kuzingatia uendelevu”, tunatoa huduma ya nishati ya mafuta inayokidhi mahitaji ya wateja wetu, washirika na jamii kwa ujumla huku tukilinda mazingira na kuendeleza usalama. Tembelea tovuti yetu kujifunza zaidi kuhusu huduma zetu, miradi yetu, na dhamira yetu ya ubora. Kwa pamoja, tunajenga mustakabali ulio bora zaidi na wenye uhakika wa nishati kwa Tanzania na zaidi ya hapo. "Kuwezesha Nishati, Kuchochea Ukuaji"

Habari Mpya

Matukio Mapya

Matangazo Mapya

Video Mpya

Picha Mjongeo
Baadhi ya Matukio na Habari katika video

Shuhuda

Jane Doe

"Tunajivunia kuhakikisha wateja wetu wanapata huduma bila kikwazo kuanzia tunapopokea oda ya mteja ya bidhaa za petroli kwa usalama na kwa wakati. Tumejitolea kutoa huduma inayozingatia wateja na ya kuaminika. Timu yetu ya wataalamu waliojitolea hufanya kazi kwa bidii ili kukidhi na kuzidi matarajio yako kwa kila utoaji."

Frank Maziku
Afisa Uendeshaji Mwandamizi
Jane Doe

"Nimeweka msisitizo kwenye kutimiza maono yetu na kuona Kampuni yetu ikiongoza uuzaji wa nishati, inayochaguliwa na wengi, na inayofanya kazi kwa njia endelevu hapa nyumbani na nje ya mipaka."

Ally Marushwa
Afisa Masoko